Bwana Mungu(God) wetu amekata pingu za dhambi kwa ajili ya watu wote. Wote wanaotaabika chini ya dhambi ni watumwa. Yeye ameondoa dhambi zetu zote. Je, yupo yeyote ambaye bado anateseka kutokana na dhambi?
Inatupasa kuelewa kwamba vita vyetu dhidi ya dhambi vimekwisha. Hatutateseka tena kamwe kutokana na dhambi. Utumwa wetu wa dhambi ulikoma Yesu alipotukomboa; dhambi zote zilikoma hapo hapo. Dhambi zetu zote zimefanyiwa upatanisho na Mwana Wake. Mungu(God) alilipia dhambi zetu zote kupitia Yesu, ambaye alituweka huru, milele.
Je, unajua jinsi watu wanavyoteseka kutokana na dhambi zao? Ilianza tangu wakati wa Adamu na Hawa. Wanadamu wanateseka kutokana na dhambi walizorithi kutoka kwa Adamu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Je, Yesu alikuja kwa maji? Ndiyo, alikuja. Alikuja kwa ubatizo Wake. Maji ni ubatizo wa Yesu uliotolewa na Yohana Mbatizaji katika Mto Yordani. Ulikuwa...
Tulizaliwa duniani humu, lakini kabla ya hapo Mungu(God) alikuwa tayari anatujua. Alijua kwamba tungezalika tukiwa wenye dhambi na akatuokoa sisi sote waumini kupitia ubatizo...
Kwa nini Yesu alimwosha Petro miguu siku moja kabla ya sikukuu ya Pasaka ya Wayahudi? Alipokuwa akimwosha miguu yake, Yesu alisema, “Wewe hujui sasa;...